Psalms 51:1-3

Kuomba Msamaha

Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Baada ya kukemewa na nabii Nathani kwa kuzini na Bathsheba.

1 aEe Mungu, unihurumie,
kwa kadiri ya upendo wako usiokoma,
kwa kadiri ya huruma yako kuu,
uyafute makosa yangu.
2 bUnioshe na uovu wangu wote
na unitakase dhambi yangu.

3 cKwa maana ninajua makosa yangu,
na dhambi yangu iko mbele yangu daima.
Copyright information for SwhNEN